Top Songs By Ambassadors of Christ Choir
Similar Songs
Lyrics
Zipo sheria pia amri za barabarani zitupasazo kuzitii tukiwa
safarini, kinachoshangaza muda mwingi tunasahau kuwa hizo amri zipo
kwa usalama wetu, ndio sababu unawaona madereva wakiendesha kwa
kuchungana na polisi, mwendo mkali bila kujali chochote,
maisha yake hata maisha ya wengine,
pale atapoona askari kwa mbali atajifanya kuzijali amri na sheria
kusudi ampendeze askari huyo ila sio kwamba ajiepushe na ajali,
ivyo divyo ilivyo sheria ya Mungu iko kwa usalama wetu Mungu mwenyewe
aimsaidii kwalolote ila nikwa faida yetu lakini siku hizi za mwisho
yapo mafundisho yaa kwamba amri zake Mungu hazifai tena
usidanganyike ndugu msafiri mwenzangu
bila amri ya Mungu atutafika salamaaaa.
Katika safari hii ya wokovu twahitaji mwongozo tuwekwe sawa na jamii
ya mbinguni kama ni kweli twaudhamini wokovu ule basi tutazishika
amri kwa usafi wetu,
kama ni kuiba madhara yake twayajua jeee kuzini matunda yake yako
wazi usidanganye kumbuka pale ulipodanganya na jinsi ulikovyosa amani
moyoni jambo hili li wazi kwamba jamii iliyo yote huwa na utamaduni
pia desturi yake kwahiyo kazi yake amri na
ile sheria ni kutuzoeza na utamaduni wa mbinguni.
Dalili moja kwabma unampenda Bwana utawafundisha watu kuzitii amri
zake hata Bwana mwenyewe kwa kinywa chake asema kama kweli mwanipenda
mtaztii amri zangu,
hivo yatupasa wote tulokombolewa kujizoeza nayo desturi ya nyumbani
punde safari itafikia mwisho wake,
anayo heri atakayefikia salama wewe uhubirie neno ni kama dereva tena
wale wafuasi wako ni abiria wapaswa kuzidhamini
sheria za huku njiani ili ufike salama na abiria .
Lyrics powered by www.musixmatch.com