Lyrics
Nilikuwa na rafiki yangu
Rafiki Pesa
Tulipendana sana
Maisha yetu yalikuwa mazuri
Nitakacho hunipatia
Nilikuwa na rafiki yangu
Rafiki pesa
Tulipendana sana
Maisha yetu yalikuwa mazuri
Nitakacho hunipatia
Nikitaka nyumba nzuri alikuwa anijengea
Nikitaka gari nzuri alikuwa aniletea
Nikitaka nguo nzuri anakimbia dukani aniletea
Nikitaka suti nzuri alikuwa aniletea
Nikitaka wanawake anakimbia Florida aniletea
Nikitaka kunywa beer alikuwa aniletea
(Instruments)
Siku moja nilishikwa na ugonjwa mbaya sana
Nikapelekwa kwa madakitari ugonjwa huo haukupona
Waliposhindwa nikarudishwa nchini kwetu nyumbani kwangu
Nikalazwa kitandani kwangu
Nilikuwa naumwa sana
Siku moja Rafiki Pesa akaja kwangu kunitazama
Akaniambia
Rafiki yangu pole sana kwa ugonjwa
Usijali hata ukifa nitakununulia coffin
Siku ile nilikufa Rafiki Pesa alitoroka
Watoto wangu waliteseka
Majirani waliwacheka
Pesa alithamini, sasa maisha kwisha
Utaenda wapi? Utaenda motoni
Wakati urafiki wako na bwana Pesa unapoisha
Mambo mawili anakufanyia
Anakununua kitamba cheupe na coffin ya kukuingiza ndani
(Instruments continues)
Walevi walikunywa pombe wakashindwa na kutembea
Wakitazama chini waona kuna mashimo
Wavuta bangi walivuta sana
Moshi nao ulipoganda
Hata nywele za vichwa zao wakashindwa kuzichana
Matajiri walipata pesa wakazieka kwa anasa
Nazo pesa zaendelea kuwanunulia sanduku
Matajiri walipata pesa wakazieka kwa anasa
Nazo pesa zaendelea kuwanunulia jeneza
(Instruments)
Usithamini pesa
Pesa zina mwisho, zina mwisho
Pesa zina mwisho
Raha nazo baba
Raha zina mwisho, zina mwisho
Raha zina mwisho
Shika Yesu baba
Yesu ndiye mwisho, ndiye mwisho
Yesu ndiye mwisho
Kwa wokovu Baba
Yesu ndiye mwisho, ndiye mwisho
Yesu ndiye mwisho
Kwa wokovu Baba
Yesu ndiye mwisho, ndiye mwisho
Yesu ndiye mwisho
Lyrics powered by www.musixmatch.com